RAIS John Magufuli ametengua uteuzi wa Majura Kasika, Mkuu wa Wilaya ya Malinyi, Morogoro na Mussa Mnyeti, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya hiyo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea).
Taarifa ya utenguzi huo imetolewa leo tarehe 17 Septemba 2019 na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais-Ikulu.
Kwa mujibu wa taarifa ya Msigwa, uteuzi wa viongozi hao umetenguliwa kuanzia leo, taarifa hiyo inaeleza kuwa, uteuzi wa viongozi watakaojaza nafasi hizo utafanyika baadaye.
Leave a comment