Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Askofu Ruwai’chi atolewa ICU
Habari Mchanganyiko

Askofu Ruwai’chi atolewa ICU

Spread the love

MHASHAMU Yuda Thadeus Ruwai’chi, Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Dar es Salaam, ametolewa katika chumba cha uangalizi maalumu (ICU). Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Kiongozi huyo wa kiroho mepelekwa katika wodi ya kawaida, baada ya hali yake kiafya kuanza kuimarika.

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 16 Septemba 2019, na Kitengo cha Uhusiano cha Taasisi ya mifupa (MOI).

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, jopo la wataalamu saba wanaomhudumia Askofu Ruwai’chi limemamua kumhamisha kutoka ICU kwenda wodi za kawaida, baada ya kujiridhisha na maendeleo ya afya yake.

Taarifa hiyo inaeleza kwamba, awali jopo hilo la wataalamu lilifanya tathimini ya vipimo pamoja na taarifa mbalimbali za maendeleo ya Askofu Ruwai’chi tangu alivyopokelewa na kufanyiwa upasuaji MOI tarehe 9 Septemba 2019.

“Taasisi ya MOI inawahakikishia Watanzania wote hususan waumini wa Kanisa Katoliki kwamba Askofu Ruwai’chi yuko salama na afya yake imeimarika sana hivyo waendelee kumuombea ili arejee kwenye majukumu yake,” inaeleza taarifa hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!