Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa JPM ampiga kijembe Lissu
Habari za SiasaTangulizi

JPM ampiga kijembe Lissu

Spread the love

RAIS John Magufuli amesema, Jimbo la Singida Mashariki limechelewa kupata maendeleo, kutokana na kutelekezwa na aliyekuwa mbunge wake, Tundu Lissu. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo tarehe 16 Septemba 2019, alipomuona Miraji Mtaturu (CCM), Mbunge wa Singida Mashariki katika hafla ya uzinduzi wa rada iliyosimikwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA).

Kiongozi huyo wa nchi ameeleza kuwa, baada ya jimbo hilo kumpata Mtaturu, serikali yake itashughulikia changamoto zake hususan maji na zingine.

Ametoa ameahidi hayo kufuatia ombi la Spika wa Bunge, Job Ndugai kwa serikali yake, kuhakikisha jimbo hilo linaondokana na changamoto ya uhaba wa maji.

 “….Laini pia namuona mheshimiwa wa lililokuwa jimbo limetelekezwa, lilikuwa la Tundu Lissu ameshika huyu. Safi sana, hongereni, mpigieni makofu na ameingia na kazi sababu saa nyingine kwenye majimbo yanakosa uwakilishi,” amesema na kuongeza.

“Na siku ile ulitoa maagizo mheshimiwa spika kwamba, tushughulikie miradi ya maji ya kule kama tulivyoshughulikia Dar es Salaam, nakuahidi tutashughulikia maji katika jimbo lile ili yale yaliyokuwa yamechelewa, yafike harakaharaka.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!