Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko NIDA watakiwa kuongeza ofisi za kutoa vitambulisho
Habari Mchanganyiko

NIDA watakiwa kuongeza ofisi za kutoa vitambulisho

Spread the love

MKUU wa mkoa wa Morogoro Dk. Kebwe Steven Kebwe ameiagiza ofisi ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) mkoa, kuongeza vituo vya  kutolea huduma katika wilaya zote ili kuwasaidia wananchi hasa waishio vijijini  kupata huduma hiyo kiurahisi. Anaripoti Christina Haule, Morogoro … (endelea).

Mkuu huyo wa mkoa alisema hayo jana wakati alipotembelea ofisi hizo kufuatia malalamiko yaliyotolewa kwake na wananchi juu ya kuchelewa kupata namba pamoja na vitambulisho jambo linaloleta athari za usajili wa laini za simu kwa jamii.

Alisema, licha ya zoezi hilo kuonekana likiendelea kufanywa lakini bado miezi minne tu kusitishwa kwa zoezi la usajili wa laini za simu kwa alama za vidole hapo mwezi Desemba mwaka huu, huku watu wengi wakiwa bado hawajapata.

Aidha aliitaka jamii kuwa na mwamko wa kuitumia nafasi iliyopo ya kwenda kupata huduma hiyo kwa wakati kwani kuchelewa kunaweza kuleta usumbufu baadae.

Naye John Msekwa mkazi wa Tungi alisema, serikali za mitaa zinatakiwa kuchukua nafasi yake kwa kuwatambua wakazi wa maeneo husika ili iwe rahisi kwao kupata vitambulisho bila kutegemea masharti yaliyopo.

“Nina miaka ya kuzaliwa zaidi ya 70 hapa, cheti nakipata wapi kwa sasa na nina mwezi wa sita natuafuta kitambulisho, kitambulisho changu cha kupigia kura  kimeharibika sana, kila ninapokwenda wanagoma kunisajilia laini,” alisema.

Akizungumzia hilo Afisa Usajili wa vitambulisho NIDA mkoani hapa, James Malimo alisema kuchelewa kwa upatikaji wa vitambuliso hivyo kwa baadhi ya wananchi kunatokana na wananchi wengi kushindwa kutimiza masharti yaliyowekwa na kwamba yapo maombi mbalimbali yamekwama kutokana na changamoto za wananchi kushindwa kuwasilisha vielelezo zaidi.

Hivyo aliwaasa wananchi kuhakikisha wanakamilisha masharti hayo ya vielelezo vya msingi na kuhakikisha wanavipata kwa wakati ili kuweza kukamilisha usajili na maombi yao yafanyiwe kazi kwani hawataweza kumsajili mtu bila kuwa na vielelezo ili kuepuka kuwasajili wasio watanzania.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!