Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Msani/Diwani ACT-Wazalendo atupwa jela
Habari za Siasa

Msani/Diwani ACT-Wazalendo atupwa jela

Clayton Chipando maarufu kwa jina la Baba Levo
Spread the love

MSANII wa kizazi kipya na mwanasiasa wa upinzani nchini Clayton Chipando maarufu kwa jina la Baba Levo, leo tarehe 1 Agosti 2019 amehukumiwa kwenda jela kwa miezi mitano. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Baba Levo ambaye ni Diwani wa Kata ya Mwanga Kaskazini kweneye Manispaa ya Kigoma Ujiji, mkoani Kigoma kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, amehukumiwa kifungo hicho baada ya kukutwa na hatia ya kumshambulia askari wa kikosi cha usalama barabarani mkoani humo F.8350 PC Msafiri Mponela.

Juma Ramadhani, Katibu wa ACT-Wazalendo Mkoa wa Kigoma  amethibitisha na kuongeza “bado tunafuatilia hukumu hiyo.”

Kwa mujibu wa mahakamani hao, kifungu kifungu No. 240 cha kanuni ya adhabu Sura ya 16 chapisho la mwaka 2002 ndio lililomtia hatiani Baba Levo.

Hukumu hiyo imetolewa leo na Hakimu Mkazi, Florence Ikolongo wa Mahakama ya Mwanzo iliyopo Mwandiga na kwamba, hukumu hiyo bila faini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!