Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Msani/Diwani ACT-Wazalendo atupwa jela
Habari za Siasa

Msani/Diwani ACT-Wazalendo atupwa jela

Clayton Chipando maarufu kwa jina la Baba Levo
Spread the love

MSANII wa kizazi kipya na mwanasiasa wa upinzani nchini Clayton Chipando maarufu kwa jina la Baba Levo, leo tarehe 1 Agosti 2019 amehukumiwa kwenda jela kwa miezi mitano. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Baba Levo ambaye ni Diwani wa Kata ya Mwanga Kaskazini kweneye Manispaa ya Kigoma Ujiji, mkoani Kigoma kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, amehukumiwa kifungo hicho baada ya kukutwa na hatia ya kumshambulia askari wa kikosi cha usalama barabarani mkoani humo F.8350 PC Msafiri Mponela.

Juma Ramadhani, Katibu wa ACT-Wazalendo Mkoa wa Kigoma  amethibitisha na kuongeza “bado tunafuatilia hukumu hiyo.”

Kwa mujibu wa mahakamani hao, kifungu kifungu No. 240 cha kanuni ya adhabu Sura ya 16 chapisho la mwaka 2002 ndio lililomtia hatiani Baba Levo.

Hukumu hiyo imetolewa leo na Hakimu Mkazi, Florence Ikolongo wa Mahakama ya Mwanzo iliyopo Mwandiga na kwamba, hukumu hiyo bila faini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

Habari za SiasaTangulizi

Mgawo wa umeme: Rais Samia ampa miezi sita bosi mpya TANESCO

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amempa miezi sita Mkurugenzi...

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

error: Content is protected !!