Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Msani/Diwani ACT-Wazalendo atupwa jela
Habari za Siasa

Msani/Diwani ACT-Wazalendo atupwa jela

Clayton Chipando maarufu kwa jina la Baba Levo
Spread the love

MSANII wa kizazi kipya na mwanasiasa wa upinzani nchini Clayton Chipando maarufu kwa jina la Baba Levo, leo tarehe 1 Agosti 2019 amehukumiwa kwenda jela kwa miezi mitano. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Baba Levo ambaye ni Diwani wa Kata ya Mwanga Kaskazini kweneye Manispaa ya Kigoma Ujiji, mkoani Kigoma kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, amehukumiwa kifungo hicho baada ya kukutwa na hatia ya kumshambulia askari wa kikosi cha usalama barabarani mkoani humo F.8350 PC Msafiri Mponela.

Juma Ramadhani, Katibu wa ACT-Wazalendo Mkoa wa Kigoma  amethibitisha na kuongeza “bado tunafuatilia hukumu hiyo.”

Kwa mujibu wa mahakamani hao, kifungu kifungu No. 240 cha kanuni ya adhabu Sura ya 16 chapisho la mwaka 2002 ndio lililomtia hatiani Baba Levo.

Hukumu hiyo imetolewa leo na Hakimu Mkazi, Florence Ikolongo wa Mahakama ya Mwanzo iliyopo Mwandiga na kwamba, hukumu hiyo bila faini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!