Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Dhamana ya mwandishi Kabendera Agosti 5
Habari Mchanganyiko

Dhamana ya mwandishi Kabendera Agosti 5

Erick Kabendera
Spread the love

MAOMBI ya dhamana Namba 14 ya mwaka 2019 ya mwanahabari Erick Kabendera, yanatarajiwa kusikilizwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam tarehe 5 Agosti 2019. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Uamuzi huo umetolewa leo tarehe 1 Agosti 2019 na Augustine Rwizile, Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya mawakili upande wa Jamhuri kuomba muda wa kuyapitia maombi hayo na kuwasilisha hati kinzani.

Maombi hayo ya dhamana yaliwasilishwa na mawakili wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), tarehe 31 Julai 2019 ikiwa ni siku mbili tangu Kabendera kukabidhiwa kwa Idara ya Uhamiaji akituhumiwa kuwa sio raia wa Tanzania.

Hadi sasa Kabendera anashikiliwa na Uhamiaji kwa ajili ya mahojiano kuhusu.

Katika maombi hayo, mawakili wa Kabendera, Catherine Ringo na Shilinde Swedy wameiomba mahakama iamuru mteja wao afikishwe mahakamani au apewe dhamana na polisi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!