Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa JPM aagiza mabadiliko ya haraka TAZARA
Habari za Siasa

JPM aagiza mabadiliko ya haraka TAZARA

Spread the love

RAIS John Magufuli ameagiza mchakato wa urekebishaji Sheria ya Reli inayounganisha nchi za Tanzania na Zambia (TAZARA), kufanyika haraka ili kuboresha shughuli za usafirishaji wa abiria na mizigo. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Taarifa iliyotolewa na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, inaeleza kwamba Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo tarehe 25 Julai 2019 akiwa safarini kuelekea Kisaki mkoani Morogoro kwa kutumia usafiri wa treni.

Aidha, Rais Magufuli amewaagiza viongozi wa TAZARA kuwasilisha mapendekezo yao juu ya hatua zinazopaswa kuchukuliwa ili kuboresha usafirishaji wa mizigo na abiria kupitia TAZARA.

“Rais Magufuli ameagiza mchakato wa kufanya marekebisho ya sheria hiyo uharakishwe ili juhudi za kununua injini na mabehewa zifanyike haraka,” inaeleza taarifa ya Msigwa.

Awali Buruno Chingandu, Mkurugenzi Mkuu wa TAZARA NA Fuad Abdallah, Meneja Mkuu wa TAZARA  Tanzania walimueleza Rais Magufuli kwamba mapendekezo ya mabadiliko ya sheria yamewasilishwa serikalini ili kuwezesha kila nchi kuwekeza katika TAZATA.

Viongozi hao wamesema mapendekezo hayo yana lengo la kuboresha yusafirishaji wa abiria na mizigo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!