Tuesday , 3 October 2023
Home Gazeti Habari za Siasa JPM aagiza mabadiliko ya haraka TAZARA
Habari za Siasa

JPM aagiza mabadiliko ya haraka TAZARA

Spread the love

RAIS John Magufuli ameagiza mchakato wa urekebishaji Sheria ya Reli inayounganisha nchi za Tanzania na Zambia (TAZARA), kufanyika haraka ili kuboresha shughuli za usafirishaji wa abiria na mizigo. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Taarifa iliyotolewa na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, inaeleza kwamba Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo tarehe 25 Julai 2019 akiwa safarini kuelekea Kisaki mkoani Morogoro kwa kutumia usafiri wa treni.

Aidha, Rais Magufuli amewaagiza viongozi wa TAZARA kuwasilisha mapendekezo yao juu ya hatua zinazopaswa kuchukuliwa ili kuboresha usafirishaji wa mizigo na abiria kupitia TAZARA.

“Rais Magufuli ameagiza mchakato wa kufanya marekebisho ya sheria hiyo uharakishwe ili juhudi za kununua injini na mabehewa zifanyike haraka,” inaeleza taarifa ya Msigwa.

Awali Buruno Chingandu, Mkurugenzi Mkuu wa TAZARA NA Fuad Abdallah, Meneja Mkuu wa TAZARA  Tanzania walimueleza Rais Magufuli kwamba mapendekezo ya mabadiliko ya sheria yamewasilishwa serikalini ili kuwezesha kila nchi kuwekeza katika TAZATA.

Viongozi hao wamesema mapendekezo hayo yana lengo la kuboresha yusafirishaji wa abiria na mizigo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Bilioni 6.1 kumaliza tatizo la maji Katoro-Buseresere – Geita

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa Umoja wa wanawake CCM, (UWT), Zainab Shomari...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali kupokea ndege ya 14 ya ATCL, safari kuongezeka

Spread the love  SERIKALI ya Tanzania, kesho tarehe 3 Oktoba 2023, inatarajia...

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

error: Content is protected !!