RAIS John Magufuli ameagiza mchakato wa urekebishaji Sheria ya Reli inayounganisha nchi za Tanzania na Zambia (TAZARA), kufanyika haraka ili kuboresha shughuli za usafirishaji wa abiria na mizigo. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).
Taarifa iliyotolewa na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, inaeleza kwamba Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo tarehe 25 Julai 2019 akiwa safarini kuelekea Kisaki mkoani Morogoro kwa kutumia usafiri wa treni.
Aidha, Rais Magufuli amewaagiza viongozi wa TAZARA kuwasilisha mapendekezo yao juu ya hatua zinazopaswa kuchukuliwa ili kuboresha usafirishaji wa mizigo na abiria kupitia TAZARA.
“Rais Magufuli ameagiza mchakato wa kufanya marekebisho ya sheria hiyo uharakishwe ili juhudi za kununua injini na mabehewa zifanyike haraka,” inaeleza taarifa ya Msigwa.
Awali Buruno Chingandu, Mkurugenzi Mkuu wa TAZARA NA Fuad Abdallah, Meneja Mkuu wa TAZARA Tanzania walimueleza Rais Magufuli kwamba mapendekezo ya mabadiliko ya sheria yamewasilishwa serikalini ili kuwezesha kila nchi kuwekeza katika TAZATA.
Viongozi hao wamesema mapendekezo hayo yana lengo la kuboresha yusafirishaji wa abiria na mizigo.
Leave a comment