Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wabunge Chadema, CCM walichoka gazeti la Tanzanite
Habari za Siasa

Wabunge Chadema, CCM walichoka gazeti la Tanzanite

Hussein Bashe, Mbunge wa Nzenga Vijijini (kulia) na Cecil Mwambe, Mbunge wa Ndanda (Chadema)
Spread the love

MBUNGE wa Ndanda, Cecil Mwambe (Chadema) na Mbunge wa Nzega Vijijini, Hussein Bashe wamehoji jeuri ya gazeti la Tanzanite kuwatukana watu inaipata wapi? Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Wabunge hao wameliita gazeti hilo kuwa la kihuni na lisilo na maadili kwamba, limekuwa likiwatuhumu baadhi ya watumishi mabalimbali, huku serikali ikibariki kwa kutoa matangazo katika gazeti hilo.

Cecil amedai, imekuwa ni kawaida kwa gazeti hilo kutumiwa na serikali na limekuwa likiwachafua watu bila kuchukuliwa hatua yoyote. 

Amedai kuwa, serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na CCM, imekuwa ikitumia gazeti hilo kuwapa matangazo licha ya nakala za gazeti hilo kutofika hata 2000.

Naye Bashe akitoa taarifa kwa Mwambe amesema, anachoamini kwamba CCM ni chama makini hivyo hakiwezi kutumia gazeti la kihuni tena lisilo na maadili kwasababu, limekaa kihuni.

Katika hatua nyingine ametaka kujua kama Rais John Magufuli amekuwa na lengo la kutoa vitambulisho kwa wajasiliamali au kuwauzia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!