Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko TRC yatakiwa kusafirisha mbolea kwa wingi
Habari Mchanganyiko

TRC yatakiwa kusafirisha mbolea kwa wingi

Treni ya Shirika la Reli Tanzania (TRC)
Spread the love

SHIRIKA la Reli Tanzania (TRC), limetakiwa kutoa kipaumbele cha kusafirisha mbolea nyingi kwa wakati mmoja na kwa gharama nafuu ili kumfikia mkulima kwa wakati na bei nafuu. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 10 Mei 2019 bungeni na Naibu Waziri wa Kilimo, Omari Mgumba alipojibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Taska Mbogo (CCM).

Katika swali lake, Mbogo alidai kwamba, Mkoa wa Katavi unapata mvua za masika kuanzia Septemba na Oktoba, lakini mara nyingi pembejeo zimekuwa zikichelewa kupelekwa wakati mwingine hadi Novemba.

“Je, serikali ina mpango gani wa kupeleka kwa wakati pembejeo mkoani Katavi,” ameuliza Mbogo.

Akijibu, Mgumba amesema serikali  imelielekeza Shirika la Reli Tanzania kutoa kipaumbele cha kusafirisha mbolea nyingi kwa wakati mmoja na gharama nafuu ili kumfikia mkulima kwa wakati na bei nafuu.

Amesema, serikali inakusanya mahitaji ya mbegu bora na viutilifu kutoka katika mikoa, ili kuhamasisha kampuni na wafanyabiashara kupeleka pembejeo kwa wakulima kabla ya msimu wa kilimo kuanza na wakati wa mauzo ya mazao.

“Vile vile ziada ya mbolea iliyopo nchini inaendelea kusambazwa katika maeneo mbalimbali kulingana na msimu ambapo hadi tarehe 30 Machi 2019, kulikuwa na tani 147,913 za mbolea,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

error: Content is protected !!