Saturday , 3 June 2023
Home Habari Mchanganyiko TRC yatakiwa kusafirisha mbolea kwa wingi
Habari Mchanganyiko

TRC yatakiwa kusafirisha mbolea kwa wingi

Treni ya Shirika la Reli Tanzania (TRC)
Spread the love

SHIRIKA la Reli Tanzania (TRC), limetakiwa kutoa kipaumbele cha kusafirisha mbolea nyingi kwa wakati mmoja na kwa gharama nafuu ili kumfikia mkulima kwa wakati na bei nafuu. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 10 Mei 2019 bungeni na Naibu Waziri wa Kilimo, Omari Mgumba alipojibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Taska Mbogo (CCM).

Katika swali lake, Mbogo alidai kwamba, Mkoa wa Katavi unapata mvua za masika kuanzia Septemba na Oktoba, lakini mara nyingi pembejeo zimekuwa zikichelewa kupelekwa wakati mwingine hadi Novemba.

“Je, serikali ina mpango gani wa kupeleka kwa wakati pembejeo mkoani Katavi,” ameuliza Mbogo.

Akijibu, Mgumba amesema serikali  imelielekeza Shirika la Reli Tanzania kutoa kipaumbele cha kusafirisha mbolea nyingi kwa wakati mmoja na gharama nafuu ili kumfikia mkulima kwa wakati na bei nafuu.

Amesema, serikali inakusanya mahitaji ya mbegu bora na viutilifu kutoka katika mikoa, ili kuhamasisha kampuni na wafanyabiashara kupeleka pembejeo kwa wakulima kabla ya msimu wa kilimo kuanza na wakati wa mauzo ya mazao.

“Vile vile ziada ya mbolea iliyopo nchini inaendelea kusambazwa katika maeneo mbalimbali kulingana na msimu ambapo hadi tarehe 30 Machi 2019, kulikuwa na tani 147,913 za mbolea,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Magunia 731 ya bangi yakamatwa, mamia ya hekari yateketezwa Arumeru

Spread the love  MAMIA ya magunia ya madawa ya kulevya aina ya...

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Habari Mchanganyiko

Serikali yakabidhi eneo la mahakama ya Afrika ya haki za binadamu

Spread the loveSerikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa...

Habari Mchanganyiko

Udhamini wa NMB mikutano ya ALAT wafikia 1.2 bilioni

Spread the loveBENKI ya NMB imeendelea kufanya kazi kwa karibu na Asasi...

error: Content is protected !!