Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waziri ampinga Mbunge CCM
Habari za Siasa

Waziri ampinga Mbunge CCM

Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamadi Masauni
Spread the love

NAIBU Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamadi Masauni amesema, hakuna utaratibu wa askari polisi kutoa fedha zao mfukoni kwa ajili ya chakula cha mahabusu. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Kauli hiyo aliitoa leo tarehe 2 Aprili 2019 bungeni alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Masasi, Rashid Chuachua (CCM).

Katika swali lake mbunge huyo alitaka kujua, ni lini serikali itarekebisha utaratibu uliopo ambapo askari wanalazimika kutoa pesa zao mfukoni ili kuwapa chakuka mahabusu.

Masauni amesema, utaratibu uliopo ni kwa serikali kupitia Jeshi la Polisi ina wajaibu wa kuwapatia chakula mahabusu waliopo kororkoroni.

“Ndugu wa mahabusu pia wanaruhusiwa kupeleka chakula kwa mahabusu wao ambao wapo korokoroni,” amesema Masauni.

Naibu Waziri huyo amesema, serikali inatambua uhaba wa vitendea kazi kwa Jeshi la Polisi ikiwa ni pamoja uchache wa magari na nyumba za askari.

Amesema, kwa sasa Wilaya ya Masasi ina nyumba za makazi ya askari zipatazo 15 ambazo zinaishi familia 30.

Na kwamba, ni kweli askari wengine 154 bado wanaishi uraiani lakini hata hivyo serikali itaendelea kujenga nyumba za makazi ya askari kwa awamu kwa kadri upatikanaji wa fedha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!