Wednesday , 8 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Waliouawa kanisani Sri Lanka wafika 290
Kimataifa

Waliouawa kanisani Sri Lanka wafika 290

Spread the love

MIILI ya watu waliopoteza maisha katika shambulio la kigaidi kwenye makanisa matatu na hoteli za kifahari nchini Sri Lanka, imefikia 290. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Shambulizi la mabomu katika makanisa yaliyoko Negombo, Batticaloa na Wilaya ya Colombo Kochchikade pamoja na hoteli za Shangri-La, Kingsburry na Common Grand yalitokea wakati wa ibada ya Sikuu ya Pasaka majira ya asubuhi jana tarehe 21 Aprili 2019.

Vyombo vya Habari vya Kimataifa vimeripoti kwamba, takribani watu 500 wamejeruhiwa kwenye shambulio hilo, na kwamba Jeshi la Polisi linawashikilia watu 24 wanaoshukiwa kuhusika na tukio hilo.

Taarifa za vyombo hivyo zinaeleza kwamba, mamlaka nchini Srilanka viliarifiwa wiki mbili kabla taarifa za tishio la kiusalama.

Katibu wa Masuala ya Ulinzi SriLanka, Hemasari Fernando amewataka wananchi wa taifa hilo kutovilaumu vyombo vya ulinzi na usalama kwa kutozuia shambulizi hilo, akisema kwamba licha ya uwepo wa taarifa za matishio ya kiusalama, vyombo hivyo havikudhania kama magaidi wangetekeleza katika maeneo hayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!