Tuesday , 3 October 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Waliouawa kanisani Sri Lanka wafika 290
Kimataifa

Waliouawa kanisani Sri Lanka wafika 290

Spread the love

MIILI ya watu waliopoteza maisha katika shambulio la kigaidi kwenye makanisa matatu na hoteli za kifahari nchini Sri Lanka, imefikia 290. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Shambulizi la mabomu katika makanisa yaliyoko Negombo, Batticaloa na Wilaya ya Colombo Kochchikade pamoja na hoteli za Shangri-La, Kingsburry na Common Grand yalitokea wakati wa ibada ya Sikuu ya Pasaka majira ya asubuhi jana tarehe 21 Aprili 2019.

Vyombo vya Habari vya Kimataifa vimeripoti kwamba, takribani watu 500 wamejeruhiwa kwenye shambulio hilo, na kwamba Jeshi la Polisi linawashikilia watu 24 wanaoshukiwa kuhusika na tukio hilo.

Taarifa za vyombo hivyo zinaeleza kwamba, mamlaka nchini Srilanka viliarifiwa wiki mbili kabla taarifa za tishio la kiusalama.

Katibu wa Masuala ya Ulinzi SriLanka, Hemasari Fernando amewataka wananchi wa taifa hilo kutovilaumu vyombo vya ulinzi na usalama kwa kutozuia shambulizi hilo, akisema kwamba licha ya uwepo wa taarifa za matishio ya kiusalama, vyombo hivyo havikudhania kama magaidi wangetekeleza katika maeneo hayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Urusi yafungua milango kwa nchi za Afrika

Spread the loveSERIKALI ya Urusi imefungua milango ya ushirikiano wa kiuchumi, kijamii...

Kimataifa

Wadukuzi wa Kichana waiba barua pepe 60,000 za Serikali ya Marekani

Spread the loveWADUKUZI wa kichana wamedukua barua pepe 60000 serikali ya Marekani...

Kimataifa

Putin aita vikundi vya kujitolea vita ya Ukraine

Spread the loveRAIS wa Urusi, Vladimir Putin, amefungua milango ya ushirikiano kwa...

Kimataifa

Mlipuko wa bomu waua 50 katika sherehe za Maulidi ya Mtume

Spread the loveWATU takribani 50 wamefariki dunia huku wengine 50 wakijeruhiwa katika...

error: Content is protected !!