Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CDF Venance: Tupo tayari kukabili uchochezi nchini
Habari za Siasa

CDF Venance: Tupo tayari kukabili uchochezi nchini

Venance Mabeyo, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania
Spread the love

MKUU wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Tanzania, Jenerali Venance Mabeyo (CDF) amesema, majeshi yamejipanga kukabiliana na vitendo vya uchochezi vinavyohatarisha usalama wa nchi. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Jenerali Mabeyo ametoa kauli hiyo leo tarehe 13 Aprili 2019, wakati akihutubia katika hafla ya uzinduzi wa Ofisi ya Rais, Chamwino jijini Dodoma.

“Tunaendelea kufuatila kauli tata zenye kuashiria ishara za uchochezi ndani ya nchi yetu, tuko tayari kukabiliana na vitendo vyovyote vitakavyotokana na uchochezi huo,” amesema Jenerali Mabeyo.

Aidha Jenerali Mabeyo amezungumzia migogoro inayoendelea katika baadhi ya nchi jirani, akisema kwamba jeshi liko tayari kuliinda nchi endapo migogoro hiyo itaathiri kwa namna yoyote ile Tanzania.

“Migogoro inayofukuta katika nchi jirani inaweza ika (influence ) kuleta hali isiyotabirika katika nchi yetu, nikuhakikishie mheshimiwa (Rais John Magufuli)tuko tayari kuilinda nchi yetu.

“Kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usalama tuko tayari kulinda wananchi na mali zao, na tuko mstari wa mbele kushirikiana na wenzetu,” amesema Jenerali  Mabeyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!