Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CDF Venance: Tupo tayari kukabili uchochezi nchini
Habari za Siasa

CDF Venance: Tupo tayari kukabili uchochezi nchini

Venance Mabeyo, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania
Spread the love

MKUU wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Tanzania, Jenerali Venance Mabeyo (CDF) amesema, majeshi yamejipanga kukabiliana na vitendo vya uchochezi vinavyohatarisha usalama wa nchi. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Jenerali Mabeyo ametoa kauli hiyo leo tarehe 13 Aprili 2019, wakati akihutubia katika hafla ya uzinduzi wa Ofisi ya Rais, Chamwino jijini Dodoma.

“Tunaendelea kufuatila kauli tata zenye kuashiria ishara za uchochezi ndani ya nchi yetu, tuko tayari kukabiliana na vitendo vyovyote vitakavyotokana na uchochezi huo,” amesema Jenerali Mabeyo.

Aidha Jenerali Mabeyo amezungumzia migogoro inayoendelea katika baadhi ya nchi jirani, akisema kwamba jeshi liko tayari kuliinda nchi endapo migogoro hiyo itaathiri kwa namna yoyote ile Tanzania.

“Migogoro inayofukuta katika nchi jirani inaweza ika (influence ) kuleta hali isiyotabirika katika nchi yetu, nikuhakikishie mheshimiwa (Rais John Magufuli)tuko tayari kuilinda nchi yetu.

“Kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usalama tuko tayari kulinda wananchi na mali zao, na tuko mstari wa mbele kushirikiana na wenzetu,” amesema Jenerali  Mabeyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!