Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Kituo cha kuzalisha umeme Mlandizi chateketea
Habari Mchanganyiko

Kituo cha kuzalisha umeme Mlandizi chateketea

Spread the love

KITUO cha kuzalisha na kusambaza umeme cha Mlandizi mkoani Pwani, kimteketea kwa moto leo tarehe 30 Machi 2019. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Akizungumza na MwanaHALISI ONLINE kuhusu tukio hilo, Wankyo Nyigesa, Kamanda wa Polisi Mkoani Pwani amesema, moto huo ulizuka majira ya saa 2.15 asubuhi. 

Kamanda Wankyo amesema, hadi sasa chanzo cha moto huo hakijajulikana na kwamba, moto huo umeteketeza transform moja yenye megawati 24 ambayo ilikuwa ikizalisha na kusambaza umeme katika maeneo ya Bagamoyo, Kibaha na Mloganzila.

“Nikikuwepo eneo la tukio, hakuna madhara yoyote kwa binadamu isipokuwa jenereta limeteketea.  Hadi sasa chanzo cha ajali hiyo hakijajulikana, tunasubiri matokeo ya uchunguzi wa watalaamu,” amesema Kamanda Wankyo.


                                    

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Kengold wakabidhiwa kombe NBC Championship

Spread the loveMdhamini mkuu wa Ligi Daraja la Kwanza (NBC Championship) Benki...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

error: Content is protected !!