Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli ateua Mkurugenzi Mamlaka ya Viwanja vya Ndege
Habari za Siasa

Rais Magufuli ateua Mkurugenzi Mamlaka ya Viwanja vya Ndege

Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam 'Terminal 3'
Spread the love

RAIS John Magufuli amemteua Mhandisi, Julius Ndyamukama kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA). Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Taarifa ya uteuzi huo imetolewa leo tarehe 26 Machi 2019 na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu.

Taarifa ya Msigwa inaeleza kuwa,  Mhandisi Ndyamukama anachukua nafasi ya Richard Mayongela ambaye uteuzi wake umetenguliwa na Rais Magufuli, na kutakiwa kuripoti Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mwasiliano ambako atapangiwa kazi nyingine.

“Uteuzi wa Mhandisi Ndyamukama unaanza leo tarehe 26 Machi 2019,” inaeleza sehemu ya taarifa ya Msigwa.

Kabla ya uteuzi huo Mhandisi Ndyamukama alikuwa Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) mkoani Dar es Salaam.

“Ndiye alikuwa msimamizi mkuu wa ujenzi wa majengo namba 3 (Terminal 3) ya uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam ambayo yapo hatua za mwisho kukamilika,” inaeleza zaidi taarifa hiyo ya Msigwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!