Monday , 29 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli ateua Mkurugenzi Mamlaka ya Viwanja vya Ndege
Habari za Siasa

Rais Magufuli ateua Mkurugenzi Mamlaka ya Viwanja vya Ndege

Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam 'Terminal 3'
Spread the love

RAIS John Magufuli amemteua Mhandisi, Julius Ndyamukama kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA). Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Taarifa ya uteuzi huo imetolewa leo tarehe 26 Machi 2019 na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu.

Taarifa ya Msigwa inaeleza kuwa,  Mhandisi Ndyamukama anachukua nafasi ya Richard Mayongela ambaye uteuzi wake umetenguliwa na Rais Magufuli, na kutakiwa kuripoti Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mwasiliano ambako atapangiwa kazi nyingine.

“Uteuzi wa Mhandisi Ndyamukama unaanza leo tarehe 26 Machi 2019,” inaeleza sehemu ya taarifa ya Msigwa.

Kabla ya uteuzi huo Mhandisi Ndyamukama alikuwa Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) mkoani Dar es Salaam.

“Ndiye alikuwa msimamizi mkuu wa ujenzi wa majengo namba 3 (Terminal 3) ya uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam ambayo yapo hatua za mwisho kukamilika,” inaeleza zaidi taarifa hiyo ya Msigwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

Habari za Siasa

ACT Wazalendo yaanika madudu miradi ya ujenzi, moundombinu

Spread the loveCHAMA cha ACT Wazalendo kimeeleza wasiwasi juu ya uelekeo wa...

Habari za Siasa

Samia ashuhudia utiaji saini ujenzi wa minara 758 ya bilioni 265

Spread the love  RAIS Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa kampuni za...

error: Content is protected !!