Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif: Zitto siyo mnafiki kama yule
Habari za SiasaTangulizi

Maalim Seif: Zitto siyo mnafiki kama yule

Spread the love

MAALIM Seif Shariff Hamad, mwanachama mpya wa Chama cha ACT-Wazalendo, amemweleza Zitto Kabwe kwamba sio mnafiki. Anaripoti Yusuph Katimba … (endelea).

Akikaribishwa Makao Makuu ya ACT-Wazalendo Kijitonyama jijini Dar es Salaam leo tarehe 19 Machi 2019 Maalim Seif, ambaye alikuwa Katibu Mkuu wa CUF amesema, uamuzi wa kujiunga na ACT-Wazalendo umesukumwa na mambo mengi ikiwemo uimara wa chama hicho na viongozi wake

“Zitto sio mnafiki kama yule (hakumtaja jina). Sio aina ya viongozi anayejikomba kwa wakubwa,” amesema Maalim Seif.

Kwenye mkutano huo uliotumika kumkabidhi kadi ya uanachama wa ACT- Wazalendo Maalim Seif amesema, chama hicho kina viongozi wenye ujasiri, adabu na wanaoendana na mazingira.

Akimwelezea Zitto ambaye ni Kiongozi Mkuu wa chama hicho amesema, sio kiongozi muoga jambo linalomfanya kuwa kiongozi imara kwa zama hizi.

“Zitto ni mtu makini, ni kiongozi ambaye hasemi jambo bila kufanya utafiti na pale anapomaliza utafiti wake hutoa matamko bila woga wowote,” amesema.

Ameeleza kuwa, kabla ya kufanya uamuzi wa kujiunga na ACT-Wazalendo, walifanya utafiti kwa vyama vine.

“Tulifanya utafiti Chadema, NLD, NCCR-Mageuzi na ACT-Wazalendo, tukajiridhisha na kufanya uamuzi wa kuhamia ACT- Wazalendo,” amesema.

Amefafanua kuwa, vyama vyote walivyopita kubisha hodi ili wapokewe vina ubora lakini ACT-Wazalendo waliona ndio kinachowafaa zaidi.

Maalim Seif amejiunga na ACT-Wazalendo jana terehe 18 Machi 2019.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za Siasa

Askofu Shoo awataka ACT kupigania maslahi ya Taifa, wasikubali kuhongwa

Spread the loveALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Askofu...

Habari za Siasa

Biteko aagiza waajiri kudhibiti vifo mahali pa kazi

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!