Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Makonda asema msiba wa Ruge umempa wakati mgumu
Habari Mchanganyiko

Makonda asema msiba wa Ruge umempa wakati mgumu

Spread the love

PAUL Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ameelezea namna alivyoupokea msiba wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba, akisema kuwa ulimpa wakati mgumu. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Makonda ametoa kauli hiyo wakati akizungumza katika shughuli ya kuuaga mwili wa Ruge iliyofanyika leo tarehe 2 Machi 2019 kwenye viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.

 Makonda amesema wakati anajadiliana na familia ya marehemu Ruge kuhusu nafasi ya yeye kutoa salamu za rambirambi, alikuwa na wakati mgumu sana kutokana na kutokuwa na neno la kusema kuhusu msiba huo.

 “Jana wakati tunajadiliana habari ya kutoa salamu za rambirambi kwangu nilikuwa na wakati mgumu sana, wakati mgumu sababu Ruge alikuwa zaidi ya rafiki kwangu. Familia yake ilijua jinsi tulivyokuwa karibu, na hata mambo ambayo hayakuwa na lazima kwenda katika vyombo vya habari na kuishia ngazi ya familia,” amesema Makonda na kuongeza:

“Sikutaka kuongea na vyombo vya habari siyo kwa sababu sikutaka, ila sikujua niseme nini na mpaka leo nimefika hapa asubuhi sina cha kusema na zaidi nimemsihi Mungu anipatie neno la kusema mbele za watu juu ya mapenzi mema ya Ruge kwangu lakini bado hajanipa la kusema, naendelea kumuomba akinipa neno la kusema, akinipa kibali cha kusema atanipa na neno la kusema.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!