Tuesday , 30 May 2023
Home Habari Mchanganyiko Makonda asema msiba wa Ruge umempa wakati mgumu
Habari Mchanganyiko

Makonda asema msiba wa Ruge umempa wakati mgumu

Spread the love

PAUL Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ameelezea namna alivyoupokea msiba wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba, akisema kuwa ulimpa wakati mgumu. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Makonda ametoa kauli hiyo wakati akizungumza katika shughuli ya kuuaga mwili wa Ruge iliyofanyika leo tarehe 2 Machi 2019 kwenye viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.

 Makonda amesema wakati anajadiliana na familia ya marehemu Ruge kuhusu nafasi ya yeye kutoa salamu za rambirambi, alikuwa na wakati mgumu sana kutokana na kutokuwa na neno la kusema kuhusu msiba huo.

 “Jana wakati tunajadiliana habari ya kutoa salamu za rambirambi kwangu nilikuwa na wakati mgumu sana, wakati mgumu sababu Ruge alikuwa zaidi ya rafiki kwangu. Familia yake ilijua jinsi tulivyokuwa karibu, na hata mambo ambayo hayakuwa na lazima kwenda katika vyombo vya habari na kuishia ngazi ya familia,” amesema Makonda na kuongeza:

“Sikutaka kuongea na vyombo vya habari siyo kwa sababu sikutaka, ila sikujua niseme nini na mpaka leo nimefika hapa asubuhi sina cha kusema na zaidi nimemsihi Mungu anipatie neno la kusema mbele za watu juu ya mapenzi mema ya Ruge kwangu lakini bado hajanipa la kusema, naendelea kumuomba akinipa neno la kusema, akinipa kibali cha kusema atanipa na neno la kusema.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wenye ulemavu waiomba MISA-TAN iwajengee uwezo wa uhuru wa kujieleza

Spread the love  TAASISI ya vyombo vya Habari kusini mwa Afrika (MISA-TAN)...

Habari Mchanganyiko

Wanawake wajawazito 2000 Korogwe washiriki Marathon, Mwenyekiti UWT amsifu Jokate

Spread the loveWANAWAKE wajawazito zaidi ya 2000 wilayani Korogwe mkoani Tanga wameshiriki...

Habari Mchanganyiko

Kirigini kuzikwa leo Butiama

Spread the love  MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Musoma Vijijini (1980-1985), Herman...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti

Spread the love  JESHI la Polisi Nchini limesema kuwa katika kukabiliana na...

error: Content is protected !!