Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bunge lazidi kuikaanga serikali ya Magufuli
Habari za SiasaTangulizi

Bunge lazidi kuikaanga serikali ya Magufuli

Rais John Magufuli (kulia) akiteta jambo na Spika wa Bunge, Job Ndugai
Spread the love

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, imetoa mapendekezo 19 kwa serikali, yanayohitaji kufanyiwa kazi haraka iwezekanavyo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Miongoni mwa mapendekezo yaliyotolewa na serikali, ni kilio cha ucheleweshaji katika utoaji wa fedha za miradi ya maendeleo kama zilivyoidhinishwa na Bunge. Baadhi ya maeneo yaliyotajwa, ni sekta za kilimo, uvuvi na maji.

Akizungumza wakati wa akiwasisha taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, mwenyekiti wa kamati hiyo, Mahamoud Mgimwa alisema, kitendo cha serikali cha kuchelewesha au kutopekeka kabisa fedha za maendeleo, kumesababisha matatizo makubwa kwa wananchi.

“Serikali haiwezi kuaminika mbele ya macho ya jamii, ikiwa haitatekeleza kwa vitendo ahadi yake ya kupelekaji fedha za maendeleo katika sekta muhimu kwa uhai wa wananchi wake,” ameeleza Mgimwa.

Alisema, “wala serikali haiwezi kuaminika ikiwa inatoza kodi hata kwenye bidhaa za maziwa na ikiwa haikumarisha ununuzi wa zao la korosho.”

Pamoja na mapendekezo hayo, Kamati ya Mgimwa imetaka serikali kuhakikisha kuwa fedha za bajeti ambazo zimepitishwa na Bunge zinapelekwa kunakohusika kama ilivyoahi bungeni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!