Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Bunge lazidi kuikaanga serikali ya Magufuli
Habari za SiasaTangulizi

Bunge lazidi kuikaanga serikali ya Magufuli

Rais John Magufuli (kulia) akiteta jambo na Spika wa Bunge, Job Ndugai
Spread the love

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, imetoa mapendekezo 19 kwa serikali, yanayohitaji kufanyiwa kazi haraka iwezekanavyo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Miongoni mwa mapendekezo yaliyotolewa na serikali, ni kilio cha ucheleweshaji katika utoaji wa fedha za miradi ya maendeleo kama zilivyoidhinishwa na Bunge. Baadhi ya maeneo yaliyotajwa, ni sekta za kilimo, uvuvi na maji.

Akizungumza wakati wa akiwasisha taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, mwenyekiti wa kamati hiyo, Mahamoud Mgimwa alisema, kitendo cha serikali cha kuchelewesha au kutopekeka kabisa fedha za maendeleo, kumesababisha matatizo makubwa kwa wananchi.

“Serikali haiwezi kuaminika mbele ya macho ya jamii, ikiwa haitatekeleza kwa vitendo ahadi yake ya kupelekaji fedha za maendeleo katika sekta muhimu kwa uhai wa wananchi wake,” ameeleza Mgimwa.

Alisema, “wala serikali haiwezi kuaminika ikiwa inatoza kodi hata kwenye bidhaa za maziwa na ikiwa haikumarisha ununuzi wa zao la korosho.”

Pamoja na mapendekezo hayo, Kamati ya Mgimwa imetaka serikali kuhakikisha kuwa fedha za bajeti ambazo zimepitishwa na Bunge zinapelekwa kunakohusika kama ilivyoahi bungeni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti

Spread the love  JESHI la Polisi Nchini limesema kuwa katika kukabiliana na...

KimataifaTangulizi

Mtuhumiwa wa mauaji ya halaiki ya Rwanda akamatwa Afrika Kusini

Spread the love  MMOJA wa watuhumiwa wakuu wa mauaji ya Kimbari ya...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

error: Content is protected !!