Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Sugu amshauri Rais Magufuli kumhamisha RC wa Mbeya
Habari za Siasa

Sugu amshauri Rais Magufuli kumhamisha RC wa Mbeya

Dk. Mpoki Ulisubisya, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya
Spread the love

MBUNGE wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ amesema kama angepata nafasi ya kumshauri Rais John Magufuli, angemshauri kumteua aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Dk. Mpoki Ulisubisya kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya badala ya kumteua kuwa balozi. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akizungumza Bungeni jijini Dodoma leo tarehe 30 Januari 2019 Sugu amesema Dk. Mpoki ni mchapakazi hivyo kitendo cha Rais Magufuli kumteua kuwa balozi, ni sawa na kuipeleka mbali huduma muhimu kwa taifa.

 “Kama ningeweza kumshauri rais, ningemshauri Dk. Mpoki kuliko kuwa balozi aletwe kuwa mkuu mkoa wa Mbeya kuliko kumpeleka mbali, kumpeleka mbali ni kupelekea mbali huduma kwa taifa,” amesema Sugu.

Katika hatua nyingine, Sugu ameipongeza wizara ya afya kwa kufanikisha ujenzi wa jengo la X-Ray katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya.

Aidha, ameiomba wizara ya afya kuondoa changamoto ya uhaba wa wataalamu wa afya hasa madaktari bingwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!