Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Sugu amshauri Rais Magufuli kumhamisha RC wa Mbeya
Habari za Siasa

Sugu amshauri Rais Magufuli kumhamisha RC wa Mbeya

Dk. Mpoki Ulisubisya, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya
Spread the love

MBUNGE wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ amesema kama angepata nafasi ya kumshauri Rais John Magufuli, angemshauri kumteua aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Dk. Mpoki Ulisubisya kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya badala ya kumteua kuwa balozi. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akizungumza Bungeni jijini Dodoma leo tarehe 30 Januari 2019 Sugu amesema Dk. Mpoki ni mchapakazi hivyo kitendo cha Rais Magufuli kumteua kuwa balozi, ni sawa na kuipeleka mbali huduma muhimu kwa taifa.

 “Kama ningeweza kumshauri rais, ningemshauri Dk. Mpoki kuliko kuwa balozi aletwe kuwa mkuu mkoa wa Mbeya kuliko kumpeleka mbali, kumpeleka mbali ni kupelekea mbali huduma kwa taifa,” amesema Sugu.

Katika hatua nyingine, Sugu ameipongeza wizara ya afya kwa kufanikisha ujenzi wa jengo la X-Ray katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya.

Aidha, ameiomba wizara ya afya kuondoa changamoto ya uhaba wa wataalamu wa afya hasa madaktari bingwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

Habari za Siasa

ACT Wazalendo yaanika madudu miradi ya ujenzi, moundombinu

Spread the loveCHAMA cha ACT Wazalendo kimeeleza wasiwasi juu ya uelekeo wa...

Habari za Siasa

Samia ashuhudia utiaji saini ujenzi wa minara 758 ya bilioni 265

Spread the love  RAIS Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa kampuni za...

error: Content is protected !!