Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Sugu amshauri Rais Magufuli kumhamisha RC wa Mbeya
Habari za Siasa

Sugu amshauri Rais Magufuli kumhamisha RC wa Mbeya

Dk. Mpoki Ulisubisya, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya
Spread the love

MBUNGE wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ amesema kama angepata nafasi ya kumshauri Rais John Magufuli, angemshauri kumteua aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Dk. Mpoki Ulisubisya kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya badala ya kumteua kuwa balozi. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akizungumza Bungeni jijini Dodoma leo tarehe 30 Januari 2019 Sugu amesema Dk. Mpoki ni mchapakazi hivyo kitendo cha Rais Magufuli kumteua kuwa balozi, ni sawa na kuipeleka mbali huduma muhimu kwa taifa.

 “Kama ningeweza kumshauri rais, ningemshauri Dk. Mpoki kuliko kuwa balozi aletwe kuwa mkuu mkoa wa Mbeya kuliko kumpeleka mbali, kumpeleka mbali ni kupelekea mbali huduma kwa taifa,” amesema Sugu.

Katika hatua nyingine, Sugu ameipongeza wizara ya afya kwa kufanikisha ujenzi wa jengo la X-Ray katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya.

Aidha, ameiomba wizara ya afya kuondoa changamoto ya uhaba wa wataalamu wa afya hasa madaktari bingwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!