Sunday , 5 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Vigogo wawili wasakwa kwa ununuzi haramu wa dhahabu
Habari Mchanganyiko

Vigogo wawili wasakwa kwa ununuzi haramu wa dhahabu

Madini ya dhahabu
Spread the love

NAIBU Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo ameagiza Jeshi la Polisi kuwakamata wafanyabiashara Mansoor Almasi na Jacob Mwapinga wanaotuhumiwa kufanya ununuzi haramu wa madini ya dhahabu kwenye Mgodi wa Ulata ulioko mkoani Iringa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Nyongo ametoa agizo hilo baada ya wafanyabaishara hao kukaidi wito wake pamoja na kuonana na Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela.

Katika hatua nyingine, Nyongo ameagiza jeshi la polisi kuwakamata wamiliki wa mgodi wa dhahabu wa Nyakavangala, kufuatia wamiliki hao kuwasilisha kwake taarifa isiyo sahihi kuhusu namna ya mgodi huo unavyoendeshwa,  ulipaji kodi na mrabaha wa serikali.

Nyongo yuko ziarani mkoani Iringa, ambapo katika ziara yake alizungumza na wachimgaji wadogo na mmiliki wa mgodi wa Ulata, Ibrahimu Msigwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari MchanganyikoTangulizi

Usafiri baharini wasitishwa kukwepa athari za kimbunga Hidaya

Spread the loveUSAFIRI wa baharini umesimamishwa kwa muda ili kukwepa athari za...

Habari Mchanganyiko

RPC Dodoma akabidhiwa bunduki mbili za wahalifu

Spread the love  Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa ya Kulevya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yazindua huduma maalum kwa wastaafu

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua huduma maalum kwa...

error: Content is protected !!