Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Vigogo wawili wasakwa kwa ununuzi haramu wa dhahabu
Habari Mchanganyiko

Vigogo wawili wasakwa kwa ununuzi haramu wa dhahabu

Madini ya dhahabu
Spread the love

NAIBU Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo ameagiza Jeshi la Polisi kuwakamata wafanyabiashara Mansoor Almasi na Jacob Mwapinga wanaotuhumiwa kufanya ununuzi haramu wa madini ya dhahabu kwenye Mgodi wa Ulata ulioko mkoani Iringa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Nyongo ametoa agizo hilo baada ya wafanyabaishara hao kukaidi wito wake pamoja na kuonana na Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela.

Katika hatua nyingine, Nyongo ameagiza jeshi la polisi kuwakamata wamiliki wa mgodi wa dhahabu wa Nyakavangala, kufuatia wamiliki hao kuwasilisha kwake taarifa isiyo sahihi kuhusu namna ya mgodi huo unavyoendeshwa,  ulipaji kodi na mrabaha wa serikali.

Nyongo yuko ziarani mkoani Iringa, ambapo katika ziara yake alizungumza na wachimgaji wadogo na mmiliki wa mgodi wa Ulata, Ibrahimu Msigwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!