Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Usafiri wakwamisha kesi ya Rugemalira, Seth
Habari za SiasaTangulizi

Usafiri wakwamisha kesi ya Rugemalira, Seth

Spread the love
TATIZO la usafiri limekwamisha kesi ya Harbinder Seth na mfanyabiashara James  Rugemalira iliyokuwa ikitajwa leo Alhamisi Novemba 22, 2018 lakini imeshindikana kutoka na washitakiwa hao kutokuwepo mahakamani. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi amesema kesi hiyo imeshindwa kutajwa kutokana na Rugemalira na Seth kushindwa kuwepo mahakamani kutokana na shida ya usafiri. Washtakiwa hao wanaokabiliwa na mashtaka 12 ya uhujumu uchumi ikiwamo ya utakatishaji wa fedha.

Wakili wa Serikali Emmanuel Nitume amesema mahakamani kuwa washtakiwa wote wanaokabiliwa na kesi hiyo hawapo kwa sababu kuna shida ya kusafiri, lakini pia ofisa mmoja wa Jeshi la Magereza aliyekuwepo mahakamani hapo alisisitiza jambo hilo la shida ya usafiri.

Katika maelezo yake Nitume amedai kesi hiyo ilipangwa kwa ajili ya kutajwa, upelelezi wake bado unaendelea na akaomba ipangiwe tarehe nyingine ya kutajwa. Baada ya kusikiliza maelezo hayo Hakimu Shaidi ameahirisha kesi hiyo hadi  Desemba 6, 2018.

Washtakiwa hao  wanakabiliwa na mashtaka  12 ya  uhujumu uchumi  kwa kula njama, kujihusisha na mtandao wa uhalifu, kughushi,  kutoa nyaraka za kughushi, kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu,  kutakatisha fedha  na kuisababisha hasara ya Dola 22milioni za Marekani na Sh 309,461,300,158.27.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!