Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi amesema kesi hiyo imeshindwa kutajwa kutokana na Rugemalira na Seth kushindwa kuwepo mahakamani kutokana na shida ya usafiri. Washtakiwa hao wanaokabiliwa na mashtaka 12 ya uhujumu uchumi ikiwamo ya utakatishaji wa fedha.
Wakili wa Serikali Emmanuel Nitume amesema mahakamani kuwa washtakiwa wote wanaokabiliwa na kesi hiyo hawapo kwa sababu kuna shida ya kusafiri, lakini pia ofisa mmoja wa Jeshi la Magereza aliyekuwepo mahakamani hapo alisisitiza jambo hilo la shida ya usafiri.
Katika maelezo yake Nitume amedai kesi hiyo ilipangwa kwa ajili ya kutajwa, upelelezi wake bado unaendelea na akaomba ipangiwe tarehe nyingine ya kutajwa. Baada ya kusikiliza maelezo hayo Hakimu Shaidi ameahirisha kesi hiyo hadi Desemba 6, 2018.
Washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka 12 ya uhujumu uchumi kwa kula njama, kujihusisha na mtandao wa uhalifu, kughushi, kutoa nyaraka za kughushi, kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu, kutakatisha fedha na kuisababisha hasara ya Dola 22milioni za Marekani na Sh 309,461,300,158.27.
Leave a comment