Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Msako wamiliki wa visima vya maji waja
Habari Mchanganyiko

Msako wamiliki wa visima vya maji waja

Spread the love

SERIKALI kuanza msako wa wamiliki wa visima visivyolipiwa ada ya matumizi ya maji kwa ajili ya kuwachukulia hatua za kisheria kwa kuwafikisha mahakamani. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akizungumza na wanahabari leo tarehe 19 Novemba 2018 jijini Dar es Salaam, Afisa Maji Bonde la Wami/Ruvu, Simon Ngonyani amesema watumiaji wa maji wasiofuata taratibu za kisheria, ikiwemo wamiliki wa hoteli 100, vituo vya mafuta 25 na kampuni 11 watafikishwa mahakamani.

“Hawa watu tukiwapelekea mahakamani tunacho wadai ni zaidi ya milioni 200 na kitu, ukiangalia kuna wengine wana madeni yaani mtu ana kisima miaka kumi iliyopita halipi, tuu hadi leo hizo nazo hatutamuacha nazo atalipa zote, baada ya kufanya zoezi zima tutajua tunawadai shilingi ngapi,” amesema Ngonyani.

Akielezea kuhusu ada za matumizi ya maji, Ngonyani amesema sheria inataka wamiliki wa visima kulipa ada hizo ili zisaidie kwenye masuala mbalimbali ikiwemo utafiti wa mwenendo wa maji chini ya ardhi.

“Sheria inasema hata kama umechimba mwenyewe, sheria inasema ulipe ada ya matumizi ya maji hayo ili hiyo ada itumike, kwa mfano inatakiwa kuangalia mwenendo wa maji ndani ya ardhi ikiwemo ubora wa maji. Sababu tuko karibu na bahari hivyo maji ya bahari yanaweza kupanda juu umechimba kisima leo maji mazuri, unashangaa mwaka mmoja au miaka fulani maji yana chumvi,” amesema Ngonyani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!