Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wavuvi 16 wa Tanzania kuburuzwa mahakamani Kenya
Habari za Siasa

Wavuvi 16 wa Tanzania kuburuzwa mahakamani Kenya

Spread the love

WAVUVI takribani 16 kutoka Tanzania wamekamatwa nchini Kenya Jumapili tarehe 18 Novemba 2018, kwa madai ya kuingia nchini humo kinyume na sheria na kutumia vifaa haram vya uvuvi. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Watanzania hao wanadaiwa kukamatwa katika ufukwe wa Bamgot karibu na Ziwa Victoria ulioko Kaunti ya Migori, na kupelekwa kwenye kituo cha polisi cha Macalder huku boti zao zikizuiliwa na Jeshi la Polisi.

Kamanda wa Polisi wa Kaunti ya Migori, Joseph Nthenge amesema watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani mara baada ya uchunguzi juu ya madai yao kukamilika, ambapo kwa sasa maafisa wa polisi wanawahoji.

Sekeseke la wavuvi katika nchi zinazozunguka na kutumia ziwa Victoria, limepamba moto baada ya siku za hivi karibuni, wavuvi wa Kenya wanaotumia ziwa hilo, kudaiwa kukamatwa na vyombo vya dola vya nchi za Tanzania na Uganda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!