Sunday , 2 April 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Wavuvi 16 wa Tanzania kuburuzwa mahakamani Kenya
Habari za Siasa

Wavuvi 16 wa Tanzania kuburuzwa mahakamani Kenya

Spread the love

WAVUVI takribani 16 kutoka Tanzania wamekamatwa nchini Kenya Jumapili tarehe 18 Novemba 2018, kwa madai ya kuingia nchini humo kinyume na sheria na kutumia vifaa haram vya uvuvi. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Watanzania hao wanadaiwa kukamatwa katika ufukwe wa Bamgot karibu na Ziwa Victoria ulioko Kaunti ya Migori, na kupelekwa kwenye kituo cha polisi cha Macalder huku boti zao zikizuiliwa na Jeshi la Polisi.

Kamanda wa Polisi wa Kaunti ya Migori, Joseph Nthenge amesema watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani mara baada ya uchunguzi juu ya madai yao kukamilika, ambapo kwa sasa maafisa wa polisi wanawahoji.

Sekeseke la wavuvi katika nchi zinazozunguka na kutumia ziwa Victoria, limepamba moto baada ya siku za hivi karibuni, wavuvi wa Kenya wanaotumia ziwa hilo, kudaiwa kukamatwa na vyombo vya dola vya nchi za Tanzania na Uganda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia apangua mawaziri

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan, amefanya mabadiliko madogo ya Baraza la...

Habari za Siasa

RC mstaafu afariki dunia, CCM yamlilia

Spread the loveALIYEWAHI kuwa mkuu wa mikoa ya Dodoma, Mara, Mtwara na...

Habari za Siasa

Marekani kuwekeza Dola 500 Mil kupeleka bidhaa na huduma Tanzania

Spread the loveMAKAMU wa Rais wa Marekani, Kamala Harris amesema miongoni mwa...

Habari za Siasa

Kamala ataja hatua mpya kuimarisha uhusiano wa kibiashara Tanzania, Marekani

Spread the loveKATIKA kuimaridha uhusiano wa kibiashara na kiuchumi baina ya Tanzania...

error: Content is protected !!