Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Prof. Kabudi aukimbia mtego wa Zitto
Habari za SiasaTangulizi

Prof. Kabudi aukimbia mtego wa Zitto

Spread the love

WAZIRI wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi ameshindwa kujibu kipengele B kwenye swali la Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe kuhusiana na idadi ya mashauri yaliyofunguliwa katika mahakama za kimataifa, ambayo serikali imeshinda na kushindwa. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Zitto leo tarehe 9 Novemba 2018 amehoji bungeni kuwa, “Je kuanzia mwaka 2000 hadi 2018 kumekuwa na mashauri mangapi dhidi ya Jamhuri ya Muungano, mangapi yameamuriwa, mangapi bado na mangapi Tanzania ilishinda.”

Lakini Prof. Kabudi hakujibu swali hilo, akisema kwamba ni la mtego na hivyo hatauingia kamwe mtego huo.

Prof. Kabudi ameeleza kuwa, serikali haita tamka chochote kuhusu kesi zilizofunguliwa kwenye mahakama za kimataifa, kwa kuwa ikitoa tamko na kuingia katika taarifa za bunge (Hansard) litahatarisha hoja za serikali katika kesi hizo.

“Masuala yote aliyoyasema, yale yaliyo katika mahakama za kimataifa serikali haitamka chochote. Nataka niwambie katika sheria za kimataifa tamko lolote nitakalolifanya hapa likaingia kwenye hansard litahatarisha hoja za serikali kwenye kesi hizo, na mtego huo uwe wa bahati mbaya au wa kutumwa sitaungia kamwe,” amesema Prof. Kabudi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

error: Content is protected !!