Monday , 5 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Kesi za Acacia, Serikali bado pasua kichwa
Habari za Siasa

Kesi za Acacia, Serikali bado pasua kichwa

Kampuni ya Acacia
Spread the love

SERIKALI imeeleza kuwa, kwa sasa hakuna kesi yoyote iliyofunguliwa na kampuni ya Madini ya Acacia Mining PLC katika mahakama ya kimataifa ya usuluhishi ya London (LCIA). Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akijibu swali la Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe, leo tarehe 9 Novemba 2018 bungeni jijini Dodoma, Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi amesema kuna mashauri mawili namba UN 173686 na 1736867 yaliyofunguliwa LCIA na kampuni za madini za Pangea na Bulyanhulu.

“Kwa sasa hakuna kesi yoyote katika mahakama za usuluhishi London iliyofunguliwa dhidi ya serikali na kampuni ya Acacia Mining. Shauri Na. LCIA Arbitration UN 173686 lililotajwa na shauri UN 1736867 yamefunguliwa mnamo Julai 3, 2017 na makampuni mawili ya madini ya hapa Tanzania ya Pangea Minerals ltd na Bulyanhulu Gold Mining Ltd,” amesema.

Prof. Kbaudi ameeleza kuwa,utetezi wa serikali kwenye kesi hizo umekwisha wasilishwa LCIA, ambapo makampuni hayo yanaendelea na mashauri hayo kwa madai ya kulinda masilahi ya wanahisa wao.

“Napenda kulijulisha bunge lako tukufu kwamba kwa mujibu wa masharti katika mikataba ya kimataifa, kanuni na desturi zinazosimamia mashauri ya usuluhishi kimataifa, inaelekeza masuala ya kesi yaliyopo kwenye vyombo vya usuluhishi ni siri mpaka pale mahakama au baraza husika la usuluhishi itakapotaka kuyaweka wazi,” amesisitiza Prof. Kabudi.

Katika swali lake, Zitto alihoji kuwa, kwa nini serikali ishtakiwe na kampuni hizo wakati ilikwisha fanya mazungumzo na kampuni mama ya Barrick ambayo ni mmiliki wa Acacia inayosimamia kampuni za madini za Pangea na Bulyanhulu, na serikali kuahidiwa kishika uchumba kiasi cha dola 300 Milioni (Sh. 700 Bilioni).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!