Tuesday , 30 April 2024
Home Kitengo Michezo Kocha Yanga amvaa Makambo
MichezoTangulizi

Kocha Yanga amvaa Makambo

Heritier Makambo
Spread the love

KOCHA wa Yanga, Mwinyi Zahera katika hali ya kushangaza ameonekana kutofurahishwa na kiwango cha mshambuliaji wake, Heritier Makambo katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya KMC. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Mchezo huo ulimazika kwa Yanga kuibuka na ushindi wa bao 1-0, Zahera alisema kuwa mchezaji huyo anapaswa kujituma mazoezini na kupunguza vitu vya ‘hovyo’.

“Makambo anapaswa kupunguza vitu vya hovyo kama kulala usiku sana, kutokula vizuri na anapaswa kutumika vizuri mazoezini na kama hata viacha basi hatacheza,” alisema kocha huyo.

Hata hivyo Zahera aliongezea kuwa sababu ya timu yake kuondoka na ushindi finyu katika mchezo wa leo ni kwa kuwa wachezaji waliidhalau KMC kwa kuwa imetoka ligi daraja la kwanza basi wakafikili mchezo ungekuwa mwepesi kwa upande wao.

Bao pekee la Yanga katika mchezo wa leo limefungwa na kiungo Feisal Salumu katika dakika ya 88 ya mchezo na kuipeleka timu hiyo kwenye nafasi ya pili baada ya kufikisha alama 22 nyuma ya Azam FC huku ikiwa imecheza michezo nane mpaka sasa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

Habari za SiasaTangulizi

Wizara Katiba na Sheria yaliomba Bunge Sh. 441.2 bilioni

Spread the love  WIZARA ya Katiba na Sheria imeliomba Bunge liidhinishe bajeti...

error: Content is protected !!