Tuesday , 30 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Utabiri wa Lema haukufika kwa Millya?
Habari za SiasaTangulizi

Utabiri wa Lema haukufika kwa Millya?

Spread the love

KATIKA siku za hivi karibuni, mbunge wa Arusha Mjini (CHADEMA), Gobless Lema, alijizolea umaarufu wa kutabiria wabunge wenzake, kuondoka chama hicho na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaandika Kibona Dickson … (endelea).

Mtabiri huyu ni Mjumbe wa Kamati Kuu (CC) ya chama kinachoendelea kupata maumivu ya kuondokewa na wabunge.

Mtabiri huyu wa twitter alitabiri juu ya Mbunge mmoja wa Kaskazini kuondoka, ikatimia baada ya Dk. Molleli wa Siha kuhamia CCM.

Aliendelea kuandika utabiri na uzushi wake mwingi kupitia twitter zake. Yakitimia, pengine kwa coincidence anazidi kujipatia umaarufu na kuota pembe za kuitwa mtabiri.

Jana, tumesikia “James Ole Millya amejivua uanachama wa Chadema na kujiuzulu ubunge.”

Kulingana na gazeti la  Mwananchi la mtandaoni,  Lema amesema, “Millya aliishaondoka Chadema siku nyingi na yeye  alikuwa anajua.” Lema amekiri kuwa Millya alikuwa rafiki yake.

Ninajiuliza, kwanini mtabiri huyu wa twitter kama alijua siku nyingi, kwa nini hakuandika juu ya kuondoka kwa Millya? Kwanini huyu mjumbe wa kamati kuu hakutoa taarifa hizi kwa chama chake?

Jibu ni moja: Kwamba, James ole Millya ni rafiki yake. Kazi ya Lema si kutabiria marafiki zake, bali kuwazushia, kuwagombanisha na kuwachonganisha, maadui zake ndani ya Chadema.

Niliwahi kuandika kuwa ndani ya Chadema kuna fitina, chuki na mifarakano. Ndani ya Chadema watu hawapendani. Mazingira haya yanachochea watu kukata tamaa; kuwa desperate na baadaye kuangukikia mikononi mwa CCM.

Mabingwa wa fitina chamani pia ni mabingwa wa propaganda. Wanajua kulisha watu propaganda. Kwa kila ahamaye wanataka umma uamini “amenunuliwa” bahati vijana wengi ni walaji na watafunaji wa propaganda.

Kwenye somo la elimu ya viumbe kuna kitu kinaitwa fertilization(yai kurutubishwa). Ili fertilization itokee, panahitajika mbegu ya mwanaume na yai la  kike.

Chuki, fitina na faraka ni yai ya kike +mbegu za kiume ni CCM. Kwamba mimba ya wabunge wa Chadema kuondoka inatungwa ndani ya chama kwenyenyewe, katika mazingira ya chuki, fitina na faraka. Watungishaji ni CCM.

CCM wataendelea kumwaga mbegu zao tu…….na wabunge wa Chadema wataendelea kuondoka. Njia pekee ya kuzuia wabunge, madiwani na viongozi wa chama hicho kutoondoka, ni kuangush mnara fitina na chuki ndani ya chama.

Watu aina ya Lema washughulikiwe kwa mujibu wa kanuni za chama.

Dickson Kibona

Kibonadickson@gmail.com.

Mwanaharakati huru..

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

error: Content is protected !!