MSHAMBULIAJI wa timu ya Taifa ya Argentina na klabu ya Machester City, Sergio Aguero ameungana wachezaji mahiri duniani waliotajwa kuwania tuzo ya FIFA ya Ballon d’Or. Anaripoti Gerva Lyenda … (endelea).
Aguero anaungana na Gareth Bale (Real Madrid), kipa wa Liverpool, Alisson, mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema na Edinson Cavani (PSG).
Waandaaji wa tuzo hiyo mwaka huu, wamesema watakuwa wakiwatangaza wachezaji watakaowania tuzo hiyo kwa mafungu mpaka wafike wachezaji 30.
Tuzo hiyo iliyoanza kutolewa mwaka 1956, hutolewa kwa mchezaji wa mpira wa kiume bora zaidi kila mwaka.
Sherehe ya kumtangaza mshindi itafanyika tarehe 3, Desemba jijini Paris, Ufaransa.
Leave a comment