Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Shahidi akwamisha kesi ya Halima Mdee
Habari za Siasa

Shahidi akwamisha kesi ya Halima Mdee

Ester Bulaya na Halima Mdee walipowasili kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam
Spread the love

KESI inayomkabili Mbunge wa Kawe, Halima Mdee katika Mahakama Hakimu Mkazi Kisutu,  ya kutoa lugha chafu dhidi ya Rais John Magufuli imekwama kusikilizwa leo tarehe 8 Oktoba 2018 baada ya shahidi upande wa mashtaka kushindwa kufika mahakamani. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Katika kesi hiyo, mashahidi upande wa mashtaka walitakiwa kutoa ushahidi wao, lakini hawakufika kitendo kilichosababisha upande wa mashataka kukosa shahidi na kesi hiyo kuahirishwa.

Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba alipanga tarehe 22 Oktoba  2018 kesi hiyo kuendelea kusikilizwa baada ya Wakili Mwandamizi wa Serikali, Patrick Mwita kudai kwamba shahidi waliyemtarajia kufika mahakamani hapo leo, yuko nje ya mkoa wa Dar es Salaam.

Licha ya kuiahirisha kesi hiyo, Hakimu Simba amesema kesi hiyo ifikapo mwezi Desemba mwaka huu iwe imeisha.

Mashahidi watatu akiwemo Mrakibu wa Polisi (SP) Batseba Kasanga Mkuu wa Kituo cha Polisi cha Urafiki upande wa mashtaka tayari wameshatoa ushahidi kuhusu kesi hiyo.

Mdee anadaiwa mnamo tarehe 3 Julai 2017 akiwa katika makao makuu ya Chadema Kinondoni jijini Dar es Salaam alitoa lugha chafu dhidi ya rais Magufuli.

Katika kesi hiyo, inadaiwa kuwa Julai 3, 2017 katika Makao Makuu ya Ofisi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) iliyopo mtaa wa Ufipa wilaya ya Kinondoni, Mdee anadaiwa kutamka maneno dhidi ya  Rais John Magufuli kuwa  “anaongea hovyo hovyo , anatakiwa  afungwe breki.”

Kauli hiyo inadaiwa kwamba ingeweza kusababisha uvunjifu wa amani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!