Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa China yathibitisha kumshikiria Rais wa Interpol
Kimataifa

China yathibitisha kumshikiria Rais wa Interpol

Rais wa Shirika la Polisi la Kimataifa (Interpol), Meng Hongwei
Spread the love

NCHI ya China imethibitisha kumzuia Rais wa Shirika la Polisi wa Kimataifa (Interpol), Meng Hongwei ikidai kuwa anafanyiwa uchunguzi na Tume ya Kupambana na Rushwa juu ya tuhuma ya ukiukaji wa sheria inayomkabili. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Wakati hayo yakijiri, taarifa zinaeleza kwamba Interpol imepokea barua ya kujiuzulu kwa Meng kutoka katika ofisi ya rais.

Meng ambaye mara ya mwisho kuonekana katika makao makuu ya Interpol mjini Lyon nchini Ufaransa akielekea China ilikuwa Septemba 25 2018, alitarajiwa kuachia madaraka katika shirika hilo mwaka 2020.

Rais huyo wa Interpol alichaguliwa kushika wadhifa huo mwezi Novemba mwaka 2016 ambaye alikuwa raia wa kwanza wa China kushikilia wadhifa huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!