Tuesday , 23 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa China yathibitisha kumshikiria Rais wa Interpol
Kimataifa

China yathibitisha kumshikiria Rais wa Interpol

Rais wa Shirika la Polisi la Kimataifa (Interpol), Meng Hongwei
Spread the love

NCHI ya China imethibitisha kumzuia Rais wa Shirika la Polisi wa Kimataifa (Interpol), Meng Hongwei ikidai kuwa anafanyiwa uchunguzi na Tume ya Kupambana na Rushwa juu ya tuhuma ya ukiukaji wa sheria inayomkabili. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Wakati hayo yakijiri, taarifa zinaeleza kwamba Interpol imepokea barua ya kujiuzulu kwa Meng kutoka katika ofisi ya rais.

Meng ambaye mara ya mwisho kuonekana katika makao makuu ya Interpol mjini Lyon nchini Ufaransa akielekea China ilikuwa Septemba 25 2018, alitarajiwa kuachia madaraka katika shirika hilo mwaka 2020.

Rais huyo wa Interpol alichaguliwa kushika wadhifa huo mwezi Novemba mwaka 2016 ambaye alikuwa raia wa kwanza wa China kushikilia wadhifa huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!