Sunday , 2 April 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Wafungwa wateka gereza, watoa masharti mazito
KimataifaTangulizi

Wafungwa wateka gereza, watoa masharti mazito

Pingu
Spread the love

KATIKA hali isiyo ya kawaida, wafungwa wanaoshikiliwa kwenye gereza la Juba nchini Sudan Kusini wanadaiwa kuliteka gereza hilo huku wakiwa na silaha ikiwemo bunduki na visu, wakishinikiza kuachiliwa huru kwa wafungwa wa kisiasa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kwa mujibu wa mtandao wa BBC Swahili, umeripoti kwamba wafungwa hao ambao idadi yao rasmi haijajulikana, walimzidi nguvu mlinzi wa lango la kuingilia la gereza walilokuwamo kisha kuvunja milango kwa risasi, na kufanikiwa kuchukua bunduki na visu kutoka ndani ya ghala la kuhifadhia silaha.

Wafungwa hao wanadaiwa kuchukua hatua hiyo ikiwa ni sehemu ya shinikizo kwa Rais wa Sudan Kusini, Salva Kiir la kumtaka kutekeleza ahadi yake ya kuwaacha huru wafungwa wa kisiasa. Na kwamba mamlaka nchini humo inaendelea na mazungumzo dhidi ya wafungwa hao waliojihami kwa silaha.

Jeshi la Polisi nchini humo limekanusha madai hiyo, likieleza kuwa wafungwa takribani 60 kati ya 400 walioko kwenye gereza hilo, ndiyo walioanzisha vurugu hizo na mgomo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Marekani yatia mguu maaandamano Kenya, yatoa maagizo kwa Rais Ruto, Odinga

Spread the love  Mabalozi kutoka nchi sita za Magharibi, zikiongozwa na Marekani,...

Kimataifa

Papa Francis alazwa hospitali kutokana na maambukizi ya mapafu

Spread the love  KIONGOZI wa Kanisa katoliki duniani, Papa Francis jana Jumatano...

Kimataifa

Nyumba ya babu yake Makamu wa Rais wa Marekani yatafutwa Zambia

Spread the love  KAMALA Harris, makamu wa rais wa Marekani, amepanga kutembelea...

Kimataifa

Benki ya Uswizi mbioni kuziwekea vikwazo akaunti za siri za Wachina

Spread the love  WAKATI Serikali na Benki ya Uswizi ikichukua hatua kali...

error: Content is protected !!