Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Watu 60 mbaroni kwa kuharibu miundombinu ya Tanesco
Habari Mchanganyiko

Watu 60 mbaroni kwa kuharibu miundombinu ya Tanesco

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa
Spread the love

ZAIDI ya watu 60 wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa tuhuma za uharibifu wa miundombinu ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Hayo yamesemwa leo tarehe 2 Oktoba 2018 na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamanda Lazaro Mambosasa wakati akizungumza na wanahabari.

Kamanda Mambosasa amesema watuhumiwa hao wamekamatwa katika nyakati tofauti kwenye operesheni za kusaka waharibifu wa miundombinu ya shirika hilo, zinazoendeshwa na TANESCO kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi.

Sambamba na watuhumiwa hao, Kamanda Mambosasa amesema Jeshi la Polisi linamshikilia dereva bodaboda mmoja anayefahamika kwa jina la Matthew Joseph kwa kosa la kumiliki na kuitumia katika matukio ya kihalifu, bunduki aina ya shotgun.

Amesema watuhumiwa hao wanaendelea na mahojiano na kwamba yakikamilika watachukuliwa hatua za kisheria zaidi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!