Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Michezo Nyota sita Spurs kuikosa Barcelona
Michezo

Nyota sita Spurs kuikosa Barcelona

Spread the love

KLABU ya Tottenham Hotspur ya Uingereza itawakosa wachezaji wake sita wa kikosi cha kwanza kuelekea kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya FC Barcelona utakaochezwa kesho kwenye Uwanja wa Wembely, London. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Wachezaji watakaoukosa mchezo huo wa kundi B ni Dele Alli, Mousa Dembele, Serge Aurier, Hugo Lloris, Christian Eriksen na mlinzi wa kati Jan Vertonghen ambao ni majeruhi.

Aurier ataendelea kukosekana baada ya kusumbuliwa na msuli wa nyuma ya mguu huku Dele Alli na Vertonghen wote watakuwa nje baada nao kupatwa na tatizo la misuli katika mchezo wa Ligi Kuu wiki iliyopita dhidi ya Huddersfield.

Kukosekana kwa wachezaji hao muhimu wa kikosi cha kwanza kwenye unaweza ukawa mtihani mgumu kwa kocha mkuu wa timu hiyo Mauricio Pochettino mbele ya mabingwa hao wa La Liga ambao nao hawakuwa na matokeo mazuri katika michezo miwili ya ligi iliyopita.

Spurs ambayo inakwenda kuvaana na Barcelona huku ikiwa na kumbukumbu ya kupoteza katika mchezo wao uliopita dhidi ya Inter Milan ya Italia, na kufanya kushika nafasi ya tatu kwenye kundi hilo huku ikiwa haina alama yoyote.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!