Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Watu 60 mbaroni kwa kuharibu miundombinu ya Tanesco
Habari Mchanganyiko

Watu 60 mbaroni kwa kuharibu miundombinu ya Tanesco

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa
Spread the love

ZAIDI ya watu 60 wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa tuhuma za uharibifu wa miundombinu ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Hayo yamesemwa leo tarehe 2 Oktoba 2018 na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamanda Lazaro Mambosasa wakati akizungumza na wanahabari.

Kamanda Mambosasa amesema watuhumiwa hao wamekamatwa katika nyakati tofauti kwenye operesheni za kusaka waharibifu wa miundombinu ya shirika hilo, zinazoendeshwa na TANESCO kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi.

Sambamba na watuhumiwa hao, Kamanda Mambosasa amesema Jeshi la Polisi linamshikilia dereva bodaboda mmoja anayefahamika kwa jina la Matthew Joseph kwa kosa la kumiliki na kuitumia katika matukio ya kihalifu, bunduki aina ya shotgun.

Amesema watuhumiwa hao wanaendelea na mahojiano na kwamba yakikamilika watachukuliwa hatua za kisheria zaidi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

Habari Mchanganyiko

Yara yaja na bima ya mazao kwa wakulima

Spread the love  WAKATI serikali ikiweka mikakati mbalimbali kuimarisha sekta ya kilimo...

error: Content is protected !!