Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Watu 60 mbaroni kwa kuharibu miundombinu ya Tanesco
Habari Mchanganyiko

Watu 60 mbaroni kwa kuharibu miundombinu ya Tanesco

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa
Spread the love

ZAIDI ya watu 60 wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa tuhuma za uharibifu wa miundombinu ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Hayo yamesemwa leo tarehe 2 Oktoba 2018 na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamanda Lazaro Mambosasa wakati akizungumza na wanahabari.

Kamanda Mambosasa amesema watuhumiwa hao wamekamatwa katika nyakati tofauti kwenye operesheni za kusaka waharibifu wa miundombinu ya shirika hilo, zinazoendeshwa na TANESCO kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi.

Sambamba na watuhumiwa hao, Kamanda Mambosasa amesema Jeshi la Polisi linamshikilia dereva bodaboda mmoja anayefahamika kwa jina la Matthew Joseph kwa kosa la kumiliki na kuitumia katika matukio ya kihalifu, bunduki aina ya shotgun.

Amesema watuhumiwa hao wanaendelea na mahojiano na kwamba yakikamilika watachukuliwa hatua za kisheria zaidi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

error: Content is protected !!