Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Michezo Mwina Kaduguda aitaka tena Simba
Michezo

Mwina Kaduguda aitaka tena Simba

Spread the love

BAADA kukamilika kwa zoezi la uchukuaji fomu kuwania uongozi ndani ya klabu ya Simba, kamati ya uchaguzi ndani ya klabu hiyo imetoa orodha ya majina 21 ya wanachama waliojitokeza kuwania nafasi za ujumbe wa bodi ya Ukurugenzi ndani ya klabu hiyo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Katika nafasi ya Mwenyekiti waliojitokeza ni watu wawili Swedi Khamisi na Mtemi Rmadhani, kwenye nafasi ya wajumbe kwa upande wa wanawake waliochukua fomu ni Jasmine Soudy na Asha Baraka, huku kwenye nafasi ya ujumbe waliojitokeza ni watu 17.

Waliochukua fomu za ujumbe ni Hussen Mlinga, Iddi Kajuna, Said Tuli, Zawadi Kadunda, Mohamed Wandi, Selemani Said, Abdalaah Mgomba, Christopher Mwansasu, Alfred Elia, Mwina Kaduguda, Juma Pinto, Ally Suru, Hamisi Mkoma, Abubakari Zebo, Omari Mazola, Patrick Rweyemamu na Seleman Seleman.

Kamati hiyo ya usajili pia imesema zoezi la urudishaji fomu litaanza siku ya Jumanne tarehe 11 septemba 2018 hadi Jumamosi 15 Septemba mwaka huu huku wakiambatanisha pamoja na nakala za vyeti vyao vilivyothibitishwa na vyuo husika.

Uchaguzi wa klabu hiyo unatarajiwa kufanyika Novemba 3, mwaka huu baada ya kubadilisha mfumo wa uendeshaji ndani ya klabu hiyo na kwenda kwenye mfumo wa kibiashara ambao unaoenekana kuwa na manufaa makubwa kwa klabu kiujumla.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

error: Content is protected !!