Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Kamishna wa TRA anusurika ajalini Dodoma
Habari MchanganyikoTangulizi

Kamishna wa TRA anusurika ajalini Dodoma

Kamishna wa Mamlaka ya Mapato nchini (TRA), Charles Kichere
Spread the love

KAMISHNA wa Mamlaka ya Mapato nchini (TRA), Charles Kichere amepata ajali asubuhi ya leo tarehe 11 Septemba 2018 mkoani Dodoma baada ya gari lake kugongana na gari jingine. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma, RPC Girres Muroto amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo akisema kuwa, hakuna mtu aliyepoteza maisha katika ajali hiyo au majeruhi.

Ajali hiyo imetokea eneo la Nanenane jijini Dodoma ambapo gari la serikali aina ya V8 alilokuwamo Kichere, kugongana na gari binafsi.

Chanzo cha ajali hiyo kinadaiwa kuwa, gari la serikali lilikuwa linajaribu kulipita gari jingine kwenye njia panda ya kwenda Chuo Kikuu cha Dodoma(UDOM) ambapo gari binafsi likajitokeza kwa mbele wakati likielekea UDOM.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!