Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli kuwalipa Wafanyakazi wa meli Bil 3.7
Habari za SiasaTangulizi

Rais Magufuli kuwalipa Wafanyakazi wa meli Bil 3.7

Spread the love

RAIS John Magufuli ameahidi kutoa kiasi cha Sh. 3.7 bilioni ndani ya wiki mbili, kwa ajili ya kulipa malimbikizo ya mishahara ya miezi 27 ya wafanyakazi wa Shirika la Huduma za Meli nchini (MSCL). Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Rais Magufuli ametoa ahadi hiyo leo tarehe 3 Septemba, 2018 wakati akihutubia katika hafla ya utiaji saini mikataba minne ya ujenzi wa meli mpya, chelezo pamoja na ukarabati wa meli ya MV Victoria na MV Butiama iliyo fanyika jijini Mwanza.

Aidha, Rais Magufuli amewataka wafanyakazi wa MSCL kufanya kazi kwa bidii pamoja na kuhakikisha shirika hilo linajiendesha kwa faida ikiwemo kudhibiti mianya ya upotevu wa mapato na wizi wa rasilimali za shirika ikiwemo mafuta.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli amemuagiza Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, Mhandisi Isaac Kamwele kumpandisha cheo Kaimu Mkurugenzi wa MSCL, Erick Hamissi kuwa Mkurugenzi wa shirika hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

error: Content is protected !!