Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli kuwalipa Wafanyakazi wa meli Bil 3.7
Habari za SiasaTangulizi

Rais Magufuli kuwalipa Wafanyakazi wa meli Bil 3.7

Spread the love

RAIS John Magufuli ameahidi kutoa kiasi cha Sh. 3.7 bilioni ndani ya wiki mbili, kwa ajili ya kulipa malimbikizo ya mishahara ya miezi 27 ya wafanyakazi wa Shirika la Huduma za Meli nchini (MSCL). Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Rais Magufuli ametoa ahadi hiyo leo tarehe 3 Septemba, 2018 wakati akihutubia katika hafla ya utiaji saini mikataba minne ya ujenzi wa meli mpya, chelezo pamoja na ukarabati wa meli ya MV Victoria na MV Butiama iliyo fanyika jijini Mwanza.

Aidha, Rais Magufuli amewataka wafanyakazi wa MSCL kufanya kazi kwa bidii pamoja na kuhakikisha shirika hilo linajiendesha kwa faida ikiwemo kudhibiti mianya ya upotevu wa mapato na wizi wa rasilimali za shirika ikiwemo mafuta.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli amemuagiza Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, Mhandisi Isaac Kamwele kumpandisha cheo Kaimu Mkurugenzi wa MSCL, Erick Hamissi kuwa Mkurugenzi wa shirika hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!