Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Amuua mkewe, ajinyonga
Habari Mchanganyiko

Amuua mkewe, ajinyonga

Emmanuel Nley, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora
Spread the love

SAID Ramadhan, Mkazi wa Kijiji cha Ikongoro wilayani Uyui amejinyonga baada ya kumuua mkewe Mwajuma Hussein kwa kumpiga risasi kutokana na wivu wa mapenzi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Taarifa ya tukio hilo imetolewa jana tarehe 24 Agosti, 2014 na Emmanuel Nley, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora wakati akizungumza na wanahabari.

Akizungumzia kuhusu tukio hilo, Kamanda Nley matukio hayo yalitokea Agosti 21 mwaka huu ambapo mwili wa marehemu Mwajuma Hussein uliokotwa kwenye msitu wa Isawima katika kitongoji cha Kombe kata ya Igagala mkoani Tabora.

Kamanda Nley alieleza kuwa, baada ya marehemu Ramadhan kumuua mkewe, alikimbilia porini akiwa na bunduki aina ya gobore aliyokutwa nayo ikiwa pembeni ya mti alioutumia kujinyonga.

Alisema kuwa, uchunguzi wa awali umeonyesha chanzo cha mauaji hayo ni wivu wa mapenzi kwani kabla Ramadahi ambaye sasa ni marehemu hajamuoa Mwajuma naye Marehemu alikuwa ameolewa na Jumanne Malawiro ambaye walizaa naye watoto wawili.

Alisema kuwa marehemu Ramadhan alihisi kuwa uenda mkewe bado ana mahusiano ya kimapenzi na mzazi mwenzie huyo ndipo akaamua kumuua na kisha yeye kujiua.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!